Kikao hicho ambacho kimeandaliwa na Kituo cha Utafiti wa Qur'ani na Kundi la Utafiti wa Qur'ani na Hadithi la Chuo Kikuu Cha Malaysia kitafanyika katika ukumbi wa chuo hicho. Waandaaji wa kikao hicho wamealika mashirika, jumuiya na makundi yote yanayojishughulisha na masuala ya Qur'ani Tukufu na Hadithi za Mtume (saw) kushiriki kwenye kikao hicho cha kimataifa.
Kikao hicho kitajadili masuala mbalimbali yanayohusiana na Qur'ani pamoja na Hadithi yakiwemo ya tafsiri ya Qur'ani, sheria za Kiislamu, miujiza ya Qur'ani, kutumiwa elimu na teknolojia ya kisasa katika kuhudumia Qur'ani na mbinu zinazopasa kutumiwa kwa ajili ya kukiarifisha kitabi hicho kitakatifu cha Mwenyezi Mungu.
Badhi ya malengo ya kuandaliwa kikao hicho yametajwa kuwa ni kuunganisha taasisi na mashirika yanayoshughulikia masuala ya Qur'ani, kuchunguza utafiti ambao umefanyika kuhusiana na Qur'ani, kuwatambulisha watu mashuhuri wanaohudumia Qur'ani na kutumia teknolojia ya kisasa katika kueneza mafundisho ya Qur'ani.