| Namba: 331435 | Tarehe: 2012/07/24 - 17:50 | Rejea: ABNA.ir | print |
Kosa gani wanalo Waislamu!!! Waislamu wa Myanmar wahitaji misada+ Picha |
Ripoti ya shirika la habari la Ahlul Bayt(as)-ABNA- Sanduku la kusaidia watu la Uturuki IHH limeeleza kuwa Waislamu wa Myanmar wamekabiliwa na hali ngumu kwani Nchi ya Myanamar kwa kila Muislamu huchukua kodi na kila atakae zaliwa pia ni lazima alipiwe kodi, wakimaanisha kuwa Waislamu wa Myanmar si Raiya wa Nchi hiyo kudai kuwa wao ni wahamiaji kutoka Nchi ya Bangladesh.

Aidha Nchi ya Myanmar ilisema kuwa Waislamu wa Nchi hiyo hawana haki ya kumiliki Ardhi, na mwenye kumiliki Ardhi huchukuliwa Ardhi yake kwa nguvu na hana haki ya kulima wala kufanya kazi, Waislamu hao hawana haki ya kusafiri kwenda Mkoa mwengnine na wanaotaka kusafiri lazima walipe kodi.

Aidha Waislamu wanaotaka kumiliki Duka lazima wamshirikishe Buda bila kutoa aina wowote ya hisa katika Duka hilo na faida itakayopatikana itagawanywa kwa kila mmoja 50%.

Pia moja kati ya unyama unaofanywa dhidi ya Waislamu wa Myanmar ni kwamba kila mwenye kutaka kuowa awajibika kuomba ruhusa lasivyo adhabu kali yamsubiri.
