| Namba: 331492 | Tarehe: 2012/07/24 - 22:18 | Rejea: ABNA.ir | print |
Hizbullah:Wauaji wakuu wa Waislamu wa Myanmar ni Marekani |
Ripoti ya shirika la habari la Ahlul Bayt(as)-ABNA- Hizbullah imelaani vikali vitendo vya kinyama dhidi ya Waislamu wa Myanmar na kusema kuwa vitendo hivyo vipo kinyume na haki za Binadamu na kutaka Ulimwengu kuwasaidia Waislamu hao, aidha kuutaka Ulimwengu kuhami watu hao wanaouawa bila hatia.
Ikiendelea kulaani vitendo hivyo ilisema: Nchi ya Myanmar haijatosheka na mauaji yake kwani kila siku wazidi kuuwa watu wasokuwa na hatia, kuuwa Watoto wadogo Akina Mama na kufukuzwa watu katoka katika majumba yao.
Hizbullah ilisisitiza kuwa; Mwanzo wa kuuwa na kutokomeza Dini ya Kiislamu ni pale tu Nchi ya Myanmar iliweka uhusiano wake madhubuti na Marekani na kuwa hatua ya kwanza ya kuuwa Waislamu, ila tu hatuelewi nini Marekani atapewa baada ya Mauaji haya?!!
