| Namba: 331741 | Tarehe: 2012/07/25 - 18:46 | Rejea: ABNA.ir | print |
Muamko wa Kiislamu Utulivu hakuna Bahrain katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani |
Ripoti ya shirika la habari la Ahlul Bayt(as)-ABNA- Yusuf Al Muhafidha mmoja kati ya watetezi wa haki za Binadamu Nchini Bahrain alisema: Siku ilopita mamia ya watu wa Bahrain waliandamana na kufunga barabara kuu za Nchi hiyo.
Akiendelea kusema: Maandamano ya Bahrain ni ishara ya kuonyesha kuwa Wananchi wa Nchi hiyo hasa Mashia hawapewi haki zao, na kuonyesha kuwa Mwezi huu wa Ramadhani utakuwa ni pigo kubwa kwa Utawala wa Nchi hiyo na utulivu ulokuwa Nchini humo sasa hautokwepo.
Mtetezi wa haki huyo alisema pia; Maandamano ya Bahrain ni ya amani na lengo la maandamano hayo ni kutaka wakamilishewe mahitaji yao na ni lazima Mwezi huu wa Ramadhani wa kubaliwe maombi yao, kama hawato kamilishiwa mahitaji hayo Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhani utakua adhabu kwa utawala wa Alikhalifa.
Aidha alimazia kwa kusema: Utawala wa Kifalme wa Bahrain umedai kuwa urushaji Puto katika maandamano ni marufuku kwani Puto hutumiwa katika masuala ya Kijasusi, aidha utawala huo ulidai kuwa urushaji Puto ni uchafuaji wa mazingira na hairuhusiwi kurusha Puto.